Breaking News

TIMU YA TAIFA YA AFRIKA KUSINI (BAFANA BAFANA) YAPATA KOCHA MPYA

Chama cha Soka cha Afrika Kusini (SAFA), kimemteua tena kocha Stuart Baxter kuinoa Bafana Bafana.
Kocha huyo mwenye miaka 63 aliiongoza timu ya taifa hilo kwenye mechi za kuwania kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2006 nchini Ujerumani. Baxter anachukua mikoa ya Ephraim Shakes Mashaba waliyemtimua Desemba mwaka uliopita.
Hata hivyo Baxter ataanza kukinoa kikosi hicho baada ya kumaliza majukumu ya kukinoa  kikosi cha klabu ya Super Sport kinachoshiriki Ligi Kuu nchini humo.

No comments