Breaking News

LALIGA MAMBO BADO MAGUMU MADRIDI,BARCA ZAPATA USHINDI MNONO

REAL MADRID Jana waliinyuka Sevilla 4-1 ndani ya Estadio Santiago Bernabeu Jijini Madrid na sasa kuhitaji Pointi 4 tu katika Mechi 2 walizobakiza ili kuwa Mabingwa wa LA LIGA huko Spain kwa mara ya kwanza tangu 2012.
Jana, Mabingwa Watetezi Barcelona, wakicheza Ugenini, waliiwasha Las Palmas 4-1 kwa Bao 3 za Neymar na moja la Luis Suarez na kuendelea kuongoza La Liga wakiwa Pointi sawa na Real na wao wako juu kwa ubora wa Magoli lakini wamebakisha Mechi 1 tu wakati Real wana Mechi 2.
Bao kwenye Mechi ya real na Sevilla zilifungwa na Nacho, Cristiano Ronaldo, Bao 2, na Toni Kroos.
Jumatano, Real wako Ugenini huko Estadio Balaidos kucheza Mechi yao ya Kiporo na Celta Vigo na utashindi kwao utawaweka Pointi 3 mbele ya Barca huku Mechizikibakia moja ,moja 

No comments